Jumatatu, 29 Septemba 2014

SAMAKI WA KUKAANGA (VIBUA)




MAHITAJI:

1.      Samaki 
2.      Chumvi 
3.      Tangawizi 
4.      Kitunguu swaum 
5.      Limao 
6.      Pilipili manga




HATUA YA KWANZ

Unawachukuwa samaki wako kiasi unaotaka kuwapika unawaparua magamba na kuwatoa utumbo, ukiwamaliza wote unawaosha na maji safi baada ya kuwaosha unamwaga yale maji ulooshea, unachukuwa chombo kingine kisicho na maji unawatia wale samaki wako unatia chumvi kidogo, limao, pilipili manga ilosagwa, tangawizi ilotwangwa na vitunguu swaum vya kusagwa unavichanganya vyote pamoja na samaki ili kutoa shombo kupata radha nzuri na harufu nzuri.






 HATUA YA PILI:

Baada ya kumaliza kuwaanda samaki wako unawasha jiko na kutayarisha vitu vya kukaangia samaki mafuta, kikaango, sahani ya kuwekea samaki, kijiko cha kuepulia kichujio cha kuchujia samaki baada ya kuwakaanga unawasha jiko unatenga kikaango unaweka mafuta unasubiri yachemke baada ya kuchemka unatia samaki wako kwa mpangilio ili wasishikane unawaacha baada ya muda mpka wabadilike rangi na kuwa rangi ya brown wakishabadilika rangi kuwa wa brown unawatoa unawatia kwenye chujio ili wajichuje mafuta wakivuja mafuta unawatoa unawaweka kwenye sahani samaki wako wanakuwa tayari.




 Unaweza kuwaandaa kwa kulia ugali, chips, ndizi za kukaanga au chakula chochote unachoweza kula na samaki wa kukaanga. 












Ijumaa, 26 Septemba 2014

NDIZI ZA MALINDI MBICHI


MAHITAJI:

1      Ndizi malindi
2.    Chumvi
3.      Hoho
4.     Karoti 
5.      Maji 
6.      Kitunguu 
7.      Nazi

HATUA YA KWANZA:

Unachukuwa ndizi malindi zako kiasi ulicho panga kupika unazimenya maganda kasha unaziweka kwenye chombo chenye maji masafi unaziosha mara mbili, chukuwa sufuria yako unayotaka kupikia zipange vizuri ndizi zako kwenye hiyo sufuria kwa mapishi yake hazitakiwi kukatwa unazipika hivyohivyo nzimanzima, zitenge jikoni ndizi zako weka maji kidogokulingana na kipimo cha ndizi ulizo pika funika na mfuniko vizuri hakikisha mvuke hautoki.





HATUA YA PILI:

 Baada ya muda kidogo angalia kama maji uloweka yamepunguwa unakatia karoti, hoho na kitunguu afu unafunika kwa muda kidogo chumvi utaweka ukiwa unaweka tui la nazi, andaa  nazi yako moja kuna ukimaliza chuja tui lako la naziya kwanza lile zito  ukimaliza weka tui lako la nazi kwenye ndizi kwa ajili ya kupata radha harufu nzuri na muonekano mzuri wa chakula changanya nazi yako na nazi mpaka tui lichemke ili lisikatike utapunguza moto kidogo utaacha lichemke mpka ubakie uji uji utaepua.



Ndizi zita kuwa tayari zimeiva unaweza kula kwa samaki wa kukaanga au nyama.

Jumanne, 23 Septemba 2014

CHAPATI ZA KUSUKUMA ZA NAZI



MAHITAJI:
  
1.      Unga wa ngano
2.      Chumvi 
3.      Maji 
4.      Nazi 
5.      Mafuta


HATUA YA KWANZA:

Unandaa unga wako wa ngano kilo 1 unaweka kwenye sinia kubwa kwa ajili ya kuukanda unga huo, ukishauweka kwenye sinia unatia chumvi kidogo unachanganya na unga wakati huo ulisha tengeneza tui la nazi pembeni, unapima tui la nazi  la kwanza  kwenye glasi 1 ya bilauli unamimina kwenye sinia la unga wako unachanganya tui la nazi na unga vikishachanganyika unapima glasi ingine ya maji ya baridi unaweka kwenye unga ulochanganya na tui la nazi unauchanganya unga wote mpaka uchanganyike, ukisha changanyika unaufunika pembeni.

HATUA YA PILI:

Unaandaa vifaa vya kupikia mafuta, frying pan (kikaango), sahani ya kuwekea chapatti, kijiko cha kuepulia, kibao na kisukumio, kisu na unga wa ngano kidogo. Ukishaandaa vitu vya kupikia unachukuwa unga wako ulokwisha ukanda unaukata madonge mawili, kisha unachukuwa kibao cha kuskumia unaweka unga kidongo ili kuzuiya unga uloukanda usinate kwenye kibao, unachukuwa donge moja kati ya yale uloyakata unaliweka kwenye kibao kisha unasukuma kwa muundo wa duara mpaka mpaka linakuwa na unene kiasi kisha unapaka mafuta juu ya unga ulousukuma sehemu yote kisha unanyunyizia unga wa ngano kidogo ili usinatane kisha unalizungusha ukimaliza unachukuwa kisu unakipaka unga kwenye makali ili kisinate kisha unakata vipande vipande saizi ya kati ukimaliza kukata unachukuwa donge moja moja unalikunja muundo wa duara, (kama inavyoonesha kwenye video hapo chini) unachukuwa na donge lingine unalifanya hivyohivyo ukimaliza kukunja zote unaandaa kwa ajili ya kupika unafunika pembeni ili kuandaa mandhari ya kupikia.




 HATUA YA TATU:


Unachukuwa kibao unakipaka unga kidogo kisha unachukuwa donge moja kati ya yale uloyakunjaa unalisukuma kwa duara kuhakikisha duara hilo linakuwa duara lisilopinda isiwe nzito wala nyepesi, unawasha jiko lako unakitenga kikaango juu ya jiko kikipata moto unatia mafuta kidogo hakikisha kikaango chote kina mafuta kasha unayafuta mafuta kwenye kikaango kwa tishu au kitambaa safi, afu unatia chapatti yako hakikisha moto usiwe mkali ukaunguza chapati yako unaangalia kama imebadilika rangi kuwa brown kidogo unaigeuza unatia mafuta kwa chini unakuwa unaigeuzageuza mpaka iwe na rangi ya brown, unageuza na upande wa pili unaweka mafuta unaigeuza mpaka iwe ya brown pia baada ya hapo unaitoa unaiweka kwenye sahani unachukuwa donge linguine unafanya kama ya mwanzompaka umalize zote.






 Chapati unaweza kulia na rost ya maini au nyama yoyote, maharage ya nazi hata ya mawese au chai ya maziwa na chai ya rangi na kwa muda wowote.










Ijumaa, 19 Septemba 2014

About Halawiyatvitam

INTRODUCTION:

It's all about food. You will have an opportunity of learning how to cook different cuisines from inside and outside the country.