Ijumaa, 26 Septemba 2014

NDIZI ZA MALINDI MBICHI


MAHITAJI:

1      Ndizi malindi
2.    Chumvi
3.      Hoho
4.     Karoti 
5.      Maji 
6.      Kitunguu 
7.      Nazi

HATUA YA KWANZA:

Unachukuwa ndizi malindi zako kiasi ulicho panga kupika unazimenya maganda kasha unaziweka kwenye chombo chenye maji masafi unaziosha mara mbili, chukuwa sufuria yako unayotaka kupikia zipange vizuri ndizi zako kwenye hiyo sufuria kwa mapishi yake hazitakiwi kukatwa unazipika hivyohivyo nzimanzima, zitenge jikoni ndizi zako weka maji kidogokulingana na kipimo cha ndizi ulizo pika funika na mfuniko vizuri hakikisha mvuke hautoki.





HATUA YA PILI:

 Baada ya muda kidogo angalia kama maji uloweka yamepunguwa unakatia karoti, hoho na kitunguu afu unafunika kwa muda kidogo chumvi utaweka ukiwa unaweka tui la nazi, andaa  nazi yako moja kuna ukimaliza chuja tui lako la naziya kwanza lile zito  ukimaliza weka tui lako la nazi kwenye ndizi kwa ajili ya kupata radha harufu nzuri na muonekano mzuri wa chakula changanya nazi yako na nazi mpaka tui lichemke ili lisikatike utapunguza moto kidogo utaacha lichemke mpka ubakie uji uji utaepua.



Ndizi zita kuwa tayari zimeiva unaweza kula kwa samaki wa kukaanga au nyama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni