Jumatatu, 6 Oktoba 2014

BUGGER



MAHITAJI:

1.      Unga wa ngano 
2.      Maziwa 
3.      Blue band 
4.      Hamira 
5.      Ufuta 
6.      Nyama 
7.      Ute wa yai (mayai) 
8.      Vitunguu 
9.      Nyanya 
10.  Kabeji 
11.  Hoho 
12.  Karoti 
13.  Chumvi 
14.  Mayonnaise 
15.  Kotmir 
16.  Kitunguu swaum 
17.  Tangawizi

HATUA YA KWANZA:

Unachukuwa unga wa ngano kiasi unachotaka kupika kwa siku hiyo unauweka kwenye chombo kipana au sinia safi unatia maziwa glasi 2, hamira, blue band, chumvi afu unakanda kama unavyokanda unga wa chapatti ukishamaliza unatengeneza madonge mazuri yanayo lingana afu unayapaka juu ute wa yai ili unapoweka ufuta usiweze kutoka baada ya hapo unanyunyizia ufuta juu ukimaliza unayaweka pembeni kwa muda wa dakika 5 ili yaumuke, afu unayaweka kwenye oveni kwa muda wa dakika 15 mpaka yawe ya brown baada ya hapo unayatoa.








 HATUA YA PILI:

Unachukuwa zile skonzi unazikata katikati na kisu kikali na kisafi kasha unaanda nyama ilokwisha chemshwa ikiwa imetiwa chumvi kidogo, kotmir, tangawizi na vitunguu swaum na imeshasagwa kasha unaandaa mayai yalochemshwa unayakata kwa muundo wa duara, hoho, karoti, nyanya, vitunguu maji na kabeji vyote unavikata kwa muundo wa viduara vidogo vidogo nay a kupendeza.





 HATUA YA TATU:

Unachukuwa skonzi ilokatwa katikati unaipaka mayonnaise kasha unaweka nyama ilosagwa afu unatia chizz ya siles unaweka nyanya ulokata, vitunguu maji, mayai, hoho, karoti na kabeji afu unaweka mayonnaise juu kisha unachukuwa kipande cha juu unafunika.







Bagger yako inakuwa tayari.



















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni